Ugonjwa Hatari kwa kuku COCCIDIOSIS

MAGONJWA / TIBA



 Kuku kuhara Damu

COCCIDIOSIS 

 Ugonjwa huu husababishwa na protozoa.
 Coccidiosis(kuhara damu)_ ugonjwa huu huonekana katika sura mbili.

 (1) Caecal coccidiosis ___Sura hii ya ugonjwa hushika vifaranga.

Dalili zake _Vifaranga huonekana wamezubaa, kushusha mabawa
Kuku kushusha Mabawa
 _Kinyesi kuonesha damu
Kinyesi chenye Damu
 _Vifo vingi hutokea
 _Vifaranga kushindwa kula na kunywa.
 _Damu huonekana kwa wingi katika kinyesi kabla ya kifo.

Kuku anayeumwa Kuhara Damu
 Katika sura hii Kifaranga chenye coccidiosis sio lazima kionesha dalili zote au kinyesi cha damu. Hapana unaweza kuona Vifaranga wako wamezubaa , huku wameshusha mabawa, kuharisha kijivu, ugoro, vifo vingi kila asubuhi unakuta vimekufa .
Coccidiosis faeces
Usipo kuwa makini unaweza kujiuliza ni ugonjwa gani? Kwa kuwa umezoea mpaka uione damu kwenye kinyesi ndio ujue kuwa ni coccidiosis.

Pia ni moja ya ugonjwa rafiki sana na uchafu, hivyo ugonjwa huu unapoingia bandani jitahidi sana kuzingatia usafi, na kuwa tenga wale kuku wagonjwa sana ili kudhibiti ugonjwa kuenea bandani.

 (2)Intestinal coccidiosis__ Sura hii ya ugonjwa hushika kuku wakubwa.

 Dalili zake. _Kuku kupunguza ulaji wa chakula _Kuku kupungua uzito
 _ Kuku kuangusha mabawa
 _Kuku kuharisha kijivu , ugoro na mara nyingi kinyesi kuwa na damu damu
Intestinal Coccidiosis Signs
 _ Kuku kukonda
_Utagaji wa mayai kupungua sana.

UKIUPASUA MZOGA 
1 Utumbo kuonekana na damu
Coccidiosis Postemortem
 2Utumbo butu kuwa na damu damu
3Utumbo butu kuvimba
4Utumbo sehemu za ndani kuonekana kama vile umesagika,cloaca ya kuku hubadilika rangi na kuwa na vidotidot kama vya damu tunaita [hemorrhage]

Coccidiosis

KUZUIA UGONJWA HUU:
 _ Epeka hali ya unyevu unyevu katika banda la kuku
 _Ni muhimu kizingatia hali ya usafi kwenye banda la kuku

 MATIBABU YA UGONJWA WA COCCIDIOSIS.
 _Esb3 _Anticox _Vitacox _Amprolium _[ dawa yeyote kati ya hizo]
Dawa yeyote kati ya hizo changanya na vitamin

Maoni na ushauri Whatsapp 0716326780

Ukiwa na swali comment hapo chini
..............................................................................................
Previous Post Next Post