Udhibiti wa magonjwa ya kuku



Image result for kuku pichaUdhibiti na Tiba Dhidi ya Magonjwa ya Kuku
Kuku wanaopata lishe bora, kutunzwa vizuri na kupatiwa chanjo
dhidi ya magonjwa yanayotokea mara kwa mara huwa na afya nzuri.
Ni bora kuzuia magonjwa kuliko kutibu ili kupunguza vifo na gharama.
Iwapo ugonjwa utatokea kuku wagonjwa watenganishwe na kuku
wasio wagonjwa na wapatiwe tiba.

 Kanuni muhimu za kufuata ili
kuzuia magonjwa ni:-
Banda liwe safi muda wote,
Kabla ya kuweka kuku, banda linyunyuziwe dawa ya kuua
wadau wa magonjwa mbalimbali,
Kuku wakaguliwe kila siku ili kubaini wagonjwa au wenye
matatizo, kuwatenga na kutoa taarifa kwa mtaalam wa mifugo,
Kuku wapatiwe chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali,
Watu wasiohusika wasiingie eneo la kufugia kuku bila utaratibu,
Ndege na wanyama wengine wasifike eneo la kufugia kuku,
Banda la kufugia kuku litenganishwe na mabanda ya mifugo
mingine,
Lango la kuingia katika banda la kuku liwekewe dawa ya
kukanyaga kwa wanaoingia ndani ili kuzuia kuingiza vimelea
vya wadudu wa magonjwa;na
Vifaa vya chakula na maji viwe safi wakati wote.
Dalili za Kuku Mgonjwa
Dalili za ujumla zinazoonekana kwa kuku mgonjwa ni kama
zifuatazo:-
Kuzubaa,
Kupoteza hamu ya kula,
Kujitenga na wenzake katika kundi; na
Kupunguza au kusimama kutaga.
Mfugaji anapoona mojawapo ya dalili hizo atoe taarifa kwa mtaalum wa
mifugo
Ufugaji wa Aina Nyingine za Ndege
Aina ya ndege wengine wanaofugwa nchini Tanzania ni pamoja na Bata
maji,Bata bukini, Kanga na Njiwa. Ndege hao hufugwa kwa
kiasi kidogo ukilinganishwa na kuku kwa kuwa soko lao ni dogo.
Utunzaji
wao hautofautiani sana na kuku;
Wajengewe banda la kuishi ambalo ukubwa wake utagemea idadi ya
ndege wanaofugwa,
Wapatiwe chakula chenye virutubisho na maji ya kunywa yakutosha,
Wapatiwe kinga na tiba dhidi ya magonjwa,
Bata maji na Bata bukini wajengewe bwawa lenye nafasi ya
kukutosha kwa ajili ya kuogelea; na
Njiwa wajengewe viota sehemu ya juu kama kwenye mapaa ya
nyumba.
Utunzaji wa Kumbukumbu
Utunzaji wa kumbukumbu ni muhimu sana katika ufugaji wa kuku na
ndege wengine wafugwao ili kusaidia mfugaji kujua maendeleo ya
ufugaji wake. Utaratibu wa kuweka kumbukumbu mara tukio linapotokea
ni lazima ili kuepuka kusahau.Mfugaji ahakikishe anaweka kumbukumbu
ambazo ni sahihi na zinazoeleweka.
Aina za Kumbukumbu
Kumbukumbu zinazopaswa kuwekwa ni pamoja na:-
Aina na idadi ya kuku waliopo kwenye kila kundi (mfano
vifaranga,wanaokua,wanaotaga,majogoo),
Uzalishaji wa mayai kwa kundi la kuku waliopo,
Utotoaji wa vifaranga,
Kinga na matibabu,
Mapato na matumizi,
Utagaji wa kila kuku na utunzaji (kwa kuku wa asili); na
Kumbukumbu za vifo.
Chakula na uchanganyaji wake
Chakula ndicho huchangia sana katika gharama za uzalishaji kwa
zaidi ya asilimia 60. Na gharama ya chakula huongezeka kila mwaka
kuliko hata gharama za mayai au kuku wenyewe.
Mfugaji anaweza kununua chakula kilichochanganywa au
kuchanganya mwenyewe. Ila anapaswa kuzingatia virutubisho na
viini lishe vilivyopo katika chakula hicho pia kuzingatia mahitaji ya
kuku wake.
Virutubisho vinavyotakiwa ni vingi lakini vimegawanywa katika
makundi sita ya vyakula ambavyo ni; protin, wanga, mafuta,
madini,vitamini na maji.
Protini inahitajika kujenga mwili wa kuku.
 Ni muhimu kwa ukuaji wa kuku, uzalishaji wa mayai na kuimarisha afya. Wanga na mafuta
vinahitajika ili kuupa mwili nguvu na joto na kuwezesha mwili kufanya
kazi zake ipasavyo. Vitamini vinahitajika ili kumwezesha mwili wa
kuku kufanya kazi zake vizuri. Madini yanahitajika ili kuimarisha
mifupa na uzalishaji.

Previous Post Next Post