Hatua za muhimu
katika uchimbaji wa bwawa
- Fyeka mahali pa kujenga bwawa.
- Pima bwawa na weka mambo.
- Ondoa udongo wa juu (mbolea, mchanga, mizizi n.k.) na weka pembeni.
- Chimba msingi wa kuta; upana futi 1 na kina futi 1½.
- Jaza huo msingi kwa udongo wa mfinyanzi na kuushindilia. Hii itasaidia kupunguza kunywea kwa maji.
- Anza kuchimba bwawa na kujenga kuta kwa kutumia udongo tu (bila mchanga, mawe, miti, mizizi n.k.) ili kupunguza kunywea kwa maji kutoka bwawani baada ya kulijaza.
- Shindilia kikamilifu udongo unaowekwa kwenye kuta.
- Jaribu kusawazisha juu ya kuta na chonga kuta ziwe na mtelemko wa kiasi, zisiwe wima kwani zitamomonyoka kirahisi.
- Chonga sakafu ya bwawa kwa kuiwekea mteremko wa kiasi kutoka upande wenye kina kifupi kwenda upande wenye kina kirefu..
- Weka bomba la kuingizia maji na bomba la kuondolea maji bwawani.
- Rudishia udongo wa juu uliouondoa hapo awali kwenye kuta za bwawa.
- Panda majani yanayotambaa kama mbudu ukutani kuzuia mmomonyoko.
- Jenga wigo wa kuweka mbolea ya samadi au Mbuji ndani yake
- Jenga uzio, seng’enge au panda miti yenye miba kuzunguka bwawa kuzuia maadui wa samaki kuingia bwawani.
- Tawanya mbolea na majivu chini ya bwawa ili kuua wadudu wanaoweza kuwamo ndani ya bwawa kabla ya samaki kupandwa bwawani.
- Baada ya hatua hizo kukamilika, sasa jaza maji bwawani.
Tags:
UFUGAJI SAMAKI