Ujenzi wa bwawa la samaki

MAMBO MUHIMU KATIKA KUCHAGUA ENEO LA KUJENGA BWAWA

1.    Maji ya kutosha ni yale yanayoweza kujaza bwawa lako ndani ya siku chache. Pia maji hayo yawe ni ya kuaminika ili wakati unapoyahitaji, yapatikane. Chanzo chaweza kuwa mto au chemichemi. (Maji ya mvua hayaaminiki, wakati yale ya bomba ni ya ghali sana kutokana na kuyalipia kwa mamlaka husika)

2.    Udongo unaofaa ni ule unaotuamisha maji, kama vile wa mfinyanzi au mchanganyiko wa mfinyanzi na tifutifu. Mchanga mtupu haufai kwani huruhusu maji kunywea kirahisi.

3.    Mteremko ni vema usiwe mkali sana, ila uwezeshe maji kutiririka kuingia na kutoka bwawani. Eneo la tambarare kabisa si zuri sana, kwani utafanya uchimbaji wa bwawa kuwa kama kisima na haitakuwa rahisi kuondoa maji toka bwawani itakapo hitajika  ambalo si zuri kwa ufugaji bora wa samaki.

4.    Ni vizuri eneo liwe karibu na nyumbani ili kudhibiti wezi na maadui wa samaki, pia huwezesha kutoa huduma kwa urahisi.


CHAGUO LA UMBO NA UKUBWA WA BWAWA
1.    Umbo na ukubwa wa bwawa hutegemea sura na mwinuko wa eneo husika na eneo alilonalo mfugaji.
2.    Kwa kawaida umbo lolote hufaa kwa uchimbaji wa bwawa, lakini, ili kurahisisha uvunaji, umbo mraba au mstatili upendekezwa zaidi.
3.    Vile vile, ukubwa wa bwawa hutegemea ukubwa wa eneo husika, uwingi wa maji na uwezo wa mkulima.
4.     Bali, ili kupata pato la kuridhisha na kurahisisha utoaji huduma kama vile kulisha, inapendekezwa kuwa ukubwa wa bwawa ni vema liwe na upana wa kati ya mita 10 na mita 20 na urefu wa kati ya mita 20 na mita 30. Umbo la mraba au mstatili huvutuia zaidi.
Previous Post Next Post