FAHAMU DALILI ZA UKOSEFU VITAMINI KATIKA KUKU.
Ulinganifu na aina nyingine ya vyakula vya kuku, kama vile
protini, wanga, mafuta, madini n.k ambavyo vinaweza kutengenezwa mwilini,
- Vitamini K ambayo hutengenezwa katika utumbo wa kuku, na
- Vitamini C hutengenezwa na mwili wa kuku. Vitamini zingine hazitengenezwi mwilini bali ni lazima kuku azipate kutoka kwenye chakula au apewe vitamini zilizotengenezwa viwandani, na zinahitajika katika kiwango kidogo sana mwilini.
Kuna makundi mawili ya vitamini, nayo
ni:-
a/ Vitamini zinazoyeyuka kwenye
mafuta (fat soluble vitamins), ambazo ni vitamini A, D, E na K.
b/ Vitamini zinazoyeyuka kwenye maji
(water soluble vitamins) ambazo ni vitamini C, B1, B2, B12 na nyingine
nyingi.
Kuku huhitaji vitamini zote hizo
kwenye chakula, vitamini hizi zote ispokuwa moja (vitamini B12) zikizidi
mwilini huondolewa kupitia mkojo. Vitamini B12 inaweza kuhifadhiwa mwilini. Kwa
maana hiyo vitamini hizo ni lazima ziwe katika chakula kinacholiwa kila siku
(daily diet).
Maelezo haya yanaonesha kuwa kuku
anahitaji vitamini 14, kwani vitamini C hutengenezwa mwilini. Ingawa vitamini K
nayo hutengenezwa lakini haitoshelezi.
Vitamini C
Husaidia kifaranga kilicho ndani ya
yai kukua, mifupa ya kifaranga kuumbika na kukua vizuri, pia mafuta kusambaa
vizuri mwilini.
Viatamini A
Huhitajika kwa kiwango kidogo sana
katika chakula cha kuku, lakini kiasi hicho kidogo ni muhimu sana kwa kuku ili
aweze kukua, kutaga mayai mazuri, mayai yaanguliwe vizuri na macho yaweze kuona
vizuri.
Dalili za Upungufu wa vitamini A mwilini.
- Kuku hukawia kukua.
- Kuku huwa dhaifu na mwenye manyoya yasiyo na mpangilio.
- Macho hayaoni vizuri.
- Utagaji usioridhisha.
- Mayai yatagwayo hayaanguliwi vizuri.
- Mayai huwa na doa au madoa madoa ya damu ndani yake (blood spots in eggs)
- Kukishwa kujikinga na maradhi ipasavyo.
- Kukonda.
- Manyoya hayaoti ipasavyo (poor featherin
Tags:
UFUGAJI KUKU