UFUGAJI
KONDOO
Kama walivyo mbuzi, kondoo pia
wanaweza kufugwa na wafugaji wadogo wadogo na kwenye eneo dogo ambalo hutumika
kwa kilimo pia. Kwa kuzingatia yafuatayo, mfugaji wa kondoo ataweza kuwa na
ufanisi mzuri.
Kondoo hupenda kujilisha kwenye makundi
Kondoo hupenda kujilisha kwenye makundi
Kondoo hupenda kujilisha kwenye makundi
Kondoo hupenda kujilisha kwenye makundi
Banda la kondoo
Banda na malazi ni lazima yawe mazuri
na
v Lenye nafasi ya kupitisha hewa vizuri,
v Linaloweza kuwakinga mifugo dhidi ya mvua, jua na upepo.
v Sakafu iliyo nyanyuka ni nzuri zaidi.
Sehemu ya mbele ya banda iwe na uwazi.
Sehemu ya mbele ya banda iwe na uwazi.
v Inashauriwa sakafu iwe na mwinuko kidogo.
Usafi
Ni
lazima Uchafu utolewe kila siku ili kuweka banda katika hali ya usafi na ukavu
kila wakati. Hii, itasaidia kuzuia magonjwa ambayo hushambulia kondoo mara kwa
mara kama vile:
v Pneumonia
v kuoza kwato
v kupunguza uwezekano wa kuwepo wadudu nyemelezi.
Kwa kondoo wanaofugwa nusu ndani nusu nje, banda la kawaida lililoezekwa linatosha kuwasitiri kondoo nyakati za usiku. Tenga walau mita za mraba 1.5 kwa kila mnyama ili kuzuia uwezekano wa magonjwa yanayotokana na msongamano.
Kwa kondoo wanaofugwa nusu ndani nusu nje, banda la kawaida lililoezekwa linatosha kuwasitiri kondoo nyakati za usiku. Tenga walau mita za mraba 1.5 kwa kila mnyama ili kuzuia uwezekano wa magonjwa yanayotokana na msongamano.
Kwa kondoo wanaolishwa ndani(zero
grazing), inatakiwa:
1)
Sehemu kavu, banda lenye hewa na kuezekwa
vizuri (skwea mita 2)
2)
Kihondi kizuri cha kulishia ili
kufanya malisho kuwa safi na kupunguza uharibifu.
3)
Sehemu nzuri ya nje inayowafaa
kondoo kutembea.
4)
Tenga walau skwea mita 3 kwa kila
kondoo. Kila mwanakondoo anahitaji eneo la kutosha kwa ajili ya kukimbia na
kucheza.
5)
Maji safi na jiwe la chumvi vinahitajika
kuwepo wakati wote.
6)
Utahitajika kuwa na banda la ziada
ama kwa muda kwa ajili ya kondoo wenye mimba, kuzalia na kwa ajili ya
wanakondoo. Pia, kwa kondoo wanaoumwa.
Banda la uzio kwa ajili ya kondoo unaweza kuwa rahisi zaidi kwa kuwa kondoo hawaruki wala kupanda juu.
Banda la uzio kwa ajili ya kondoo unaweza kuwa rahisi zaidi kwa kuwa kondoo hawaruki wala kupanda juu.
Virutubisho kwa ajili ya kondoo
Kondoo hutumia muda mwingi wakati
wa mchana kula majani na baadaye hucheua na kutafuna. Wanapendelea zaidi kula
majani na vichaka ambavyo vina mchanganyiko wa madawa ya asili. Wanakondoo
hujifunza kutoka kwa mama zao ni nini chakula. Kama unawaanzishia aina mpya ya
chakula, lisha kwa kiasi kidogo na uweke kwenye sehemu walikozoea kulishiwa.
Kuwa makini na ukumbuke kuwa wanyama wanaopata lishe duni ni rahisi kushambuliwa na magonjwa na hawana uwezo wa kukabiliana na vimelea vya magonjwa. Uzalishaji wa maziwa pia huwa kidogo kiasi cha kufanya watoto wake kuwa dhaifu na kukua kwa shida.
Kuwa makini na ukumbuke kuwa wanyama wanaopata lishe duni ni rahisi kushambuliwa na magonjwa na hawana uwezo wa kukabiliana na vimelea vya magonjwa. Uzalishaji wa maziwa pia huwa kidogo kiasi cha kufanya watoto wake kuwa dhaifu na kukua kwa shida.
Tags:
MBINU ZA UFUGAJI