Kwa
kawaida ili kupata kuku wengi kwa muda
mfupi tetea lazima atengwe na vifaranga arudishwe kwenye kundi lenye jogoo,
atapandwe
na kurudia
kutaga mapema.
Kwa kawaida
vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na baridi,kuliwa
na wanyama wengine na magonjwa.
Ili kudhibiti
magonjwa, vifaranga wapewe chanjo dhidi ya magonjwa yafuatayo:
a. Kideri
( New castle) siku
ya 3-7 baada ya kuanguliwa, rudia baada ya wiki tatu kisha
uchanje kila
baada ya miezi mitatu.
b. Kuhara
damu au rangi ya ugoro (Coccidiosis) : Wapewe kinga kwa dawa ya
Amprolium
kwa siku 3 mfululizo wanapofikisha umri wasiku 7 baada ya kuanguliwa.
c.
Gumboro wanashusha mbawa
na kujikusanya pamoja kwa baridi, pia wanaharisha
nyeupe.Hutokea
kuanzia wiki ya 2 hadi ya 18.Wapewe chanjo siku ya 10-14
baada ya
kuanguliwa na rudia baada ya siku 28 na 42. Kwa magonjwa mengine
angalia
maelekezo sehemu ya magonjwa ndani ya mwongozo huu.
Vifaranga
wapewe chakula kilichoelezwa katika sehemu ya tatu ya kijitabu hiki na
maji safi ya
kutosha wakati wote kwa muda wa miezi miwili. Baada ya hapo wanapewa
chakula cha
kuku wanaokua.
Kuku
wakikaribia kupevuka wakiwa na miezi mitatu hadi minne tenganisha temba
na majogoo
ili kudhibiti kuku wenye uhusiano wa damu wasipandane wao kwa wao.
Wakipandana
na mayai yao yakianguliwa hawatatoka vifaranga wenye sifa nzuri mfano:
ukuaji wao
utakuwa hafifu kuliko wazazi wao, uwezo mdogo kuhimili magonjwa na
wengine
wanaweza kuwa na ulemavu.
Kumbuka;Pia
zingatia matemba hao wasipandwe na baba
yao.
Vilevile majogoo hao wasimpande mama yao.
Tags:
MBINU ZA UFUGAJI
