Ufugaji bora wa sungura
UFUGAJI WA NJE
1. Sehemu
yote izungushiwe wavu kuzuia panya
kuingia na wanyama wengine kama paka, mbwa, mwewe nk
2. Upande
mmoja uwe na mabanda, sehemu ya chakula na maji pamoja na kivuli kwa ajili ya
sungura kupumzika
3. Futi moja
chini ya udongo kuwe na zege kuzuia sungura kuchimba na kwenda mbali
4. Eneo
la wazi liwe huru na hatari zote za sumu kama dawa za kuulia wadudu au mbolea,
pia majani yaliyoota yasiwe ni yale yenye sumu (waone wataalamu wakushauri au
ng'oa yote)
MAJI
Tumia
mabakuli ya kigae, plastiki au jengea kwa saruji, maji yabadilishwe kila siku
na vyombo visafishwe kila siku.
CHAKULA
Wapewe
majani, mabaki ya mboga za jikoni baada ya kuchambuliwa, pia unaweza kuwawekea
pumba au chakula cha kuku (growers mash) kwenye vyombo maalum kama chakula
chenye virutubisho (concentrates).
USAFI
Kila siku
jaribu kuondoa uchafu kama vyakula vilivyo mwagika, na kinyesi kilichoganda
kwenya matandazio, fagia na kubadili matandazio angalau mara moja kwa wiki,
manyoya ya sungura mzazi yasiondolewe hii huonyesha kwamba anakaribia
kujifungua watoto.
DAWA
Hakikisha
wanapata dawa za minyoo kama piperazine
kila baada ya miezi mitatu, dawa za wadudu kama akheri powder zinyunyuziwe
kwenya mabanda yao kuzuia viroboto,
MIGUU
Miguu ya
sungura si kama ya wanyama wengine, nyayo zake zimefunikwa kwa manyoya,
zingatia manyoya hayanyonyoki,kama yakinyonyoka ni tatizo
Kumbuka:usithubutu
kuwapa dawa nyingine bila ushauri wa kitaalam,Antibiotics usijaribu kuwapa.
......................................................................................................................................
......................................................................................................................................
