Hatua za Tahadhari za Kuzuia Kuingia
na Kuenea kwa Magonjwa Shambani
1. Tenganisha ndege kufuatana na aina ya ndege na umri wao
2. Weka karantini kwa ndege/kuku wapya ili wachunguzwe kwa kipindi
kisichopungua wiki mbili
kabla ya kuingizwa shambani au bandani.
3. Usiruhusu tabia ya kuchangia vifaa/vyombo kama vile makasha ya
mayai, makreti ya kubebea kuku
kati ya shamba na shamba, n.k.
4. Wafanyakazi waanze kuwahudumia kuku wenye umri mdogo kabla ya
wale wenye umri mkubwa.
5. Usiruhusu watoto kucheza na kuku.
6. Jaribu kuzuia idadi ya wageni wanaoingia shambani/bandani.
7. Weka utaratibu wa kuangamiza mizoga ya kuku.
8. Anzisha programu jumuishi ya kudhibiti wadudu/wanyama
waharibifu.
9. Panga utaratibu mzuri wa kuwapa kuku huduma ya maji na kufanya
usafi.
10. Panga utaratibu mzuri wa kuzoa taka na mizoga ya kuku.
11. Panga utaratibu mzuri wa kusafisha banda na kupulizia dawa.
12. Vifaa visafishwe na kuwekwa dawa ya kuua vijidudu kabla ya
kuingizwa shambani.
13. Hakikisha magari yanapoingia shambani yanapita katika kidimbwi
chenye dawa ya kuua vimelea
vya magonjwa.
14. Hakikisha mfanyakazi anabadilisha viatu/mabuti kabla ya
kuingia katika kila banda
15. Weka taratibu nzuri za kuingia shambani, ikiwa ni pamoja na
kuhakikisha usafi wa viatu na mikono;
au wageni na wafanyakazi kubadilisha nguo/viatu
na kuvaa mabuti
Tags:
MAGONJWA YA KUKU