Sasa


Utunzaji kuku kwa makundi

Utunzaji wa Kuku kwa Makundi
https://www.animalscience.care/

Utunzaji wa Vifaranga

Malezi bora ya vifaranga ni muhimu katika ufugaji wa kuku kwa sababu

vifaranga hawana uwezo wa kustahimili mazingira wakiwa wenyewe mara

wanapoanguliwa.Ukosefu wa malezi bora husababisha vifaranga kuwa

dhaifu,kufa kwa wingi na hivyo kupunguza idadi ya kuku wa baadaye.

Malezi ya vifaranga yanaweza kufanyika kwa kutumia kuku walezi au

kutumia vifaa maalum.

Kulea Vifaranga kwa Kutumia Kuku Mlezi

Vifaranga wanaweza kulelewa na mama yao au kuku mlezi. Endapo kuku

wengi wametotoa vifaranga kwa wakati mmoja, achaguliwe kuku mlezi

aliye na uwezo wa kulea vifaranga wengi kati ya waliototoa aendelee kulea

na wengine waliototoa waachwe huru ili warudi kwenye mzunguko wa

kutaga. Kuku mmoja anaweza kulea vifaranga 20 hadi 25. Mfugaji wa

kuku,pamoja na kanuni nyingine, anapaswa kuzingatia yafuatayo:-

Kuku anayelea vifaranga atengewe chumba maalumu, apewe maji ya

kutosha na chakula chenye virutubisho muhimu,

Vifaranga wasiachiwe kutoka nje hadi watakapofika umri wa wiki 6,

Vifaranga watengwe na mama/mlezi baada ya wiki 4 kuruhusu mama

aendelee na mzunguko wa kutaga;na

Katika maeneo yenye hali ya hewa ya ubaridi vifaranga

wacheleweshwe kutenganishwa na mama/mlezi hadi wiki ya 6 au

mpaka waonekane wameota manyoya ya kutosha

Kulea Vifaranga kwa Kutumia Bruda

Bruda ni chombo/sehemu iliyoandaliwa mahusus kwa ajili ya kuwapatia

joto vifaranga badala ya mama/mlezi. Mfugaji anaweza kulea vifaranga

wengi kwa kutumia bruda ambayo ni mduara unaweza kutengenezwa kwa

kutumia mbao, karatasi ngumu au kwa kuziba pembe za chumba.Aidha,

njia hii hupunguza vifo vya vifaranga vinavyosababishwa na ndege au

wanyama hatari,huruhusu kuku kutaga mapema zaidi na kuwa na

mizunguko mingi ya utagaji (kwa kuku wanaoatamia). Vilevile, hurahisisha

udhibiti wa magonjwa.

Mfugaji anapaswa kufuata taratibu zifuatazo katika kulea vifaranga kwa

kutumia bruda:-

Kuweka vifaa vya kuongeza joto kwa mfano taa ya umeme, chemli au

jiko la mkaa. Zingatia kiwango cha joto kinachohitajika katika bruda.

Wiki ya kwanza ni 35oc, wiki ya pili ni 33oc, wiki ya tatu ni 31oc na

wiki ya nne ni 29oc,

Kuchunguza mtawanyiko wa vifaranga ndani ya bruda ili kutathimini

hali ya joto.Wakijikusanya kwenye chanzo cha joto, inaashiria kuwa

baridi imezidi hivyo joto liongezwe. Wakiwa mbali na chanzo cha joto

maana yake joto limezidi hivyo joto lipunguzwe,

Bruda iwe na sakafu yenye malalo yatokanayo na maranda ya mbao

au pumba za mpunga. Malalo yabadilishwe endapo yataonekana

yameloana,

Bruda iwekwe vifaa vya maji na chakula. Maji na chakula kiwekwe

kabla ya kuweka vifaranga,

Vifaa vya joto viwekwe ndani ya bruda masaa 6 kabla ya kuingiza

vifaranga,

Vifaranga walishwe chakula cha kuanzia gramu 12-15 kwa kipindi

cha wiki ya 2. Katika wiki ya 3 wapewe gramu 21-35 kwa kifaranga

na chakula hicho kiwepo muda wote,

Vifaranga wapatiwe vitamin, madini na dawa za kinga (antibiotics); na

Vifaranga wapatiwe chanjo kulingana na maelekezo ya mtaalamu wa

mifugo.Chanjo dhidi ya magonjwa muhimu kwa mfano,Marek’s (mara

anapototolewa), Mdondo (siku ya 3-4 na kurudiwa baada ya siku ya

21 na kila baada ya miezi 3) na Gumboro (siku ya 7na kurudia tena

siku ya 21).Wapatiwa dawa ya minyoo (wiki ya 8) na coccidiosis(wiki

ya 3-4). Siku ya 45 wapewe chanjo ya ndui ya kuku.

2. Kutunza Kuku Wanaokua (Wiki 8-18)

Utunzaji wa kundi hili unategemea mfumo unaotumika.

Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Huria

Kuku wanaofugwa katika mfumo huu wapatiwe matunzo bora

yakiwemo yafuatayo;

ü Wapewe chakula cha ziada asubuhi kabla ya kutoka na

    wanaporudi kwenye banda. Chakula hicho kinaweza kugawanywa

mara ya 2 kwa siku,

ü  Wapatiwe maji safi na ya kutosha wakati wote

ü  Wapatiwe chanjo na dawa kulingana na ushauri wa mtaalam wa

mifugo. Wiki ya kumi warudie chanjo ya mdondo, wiki ya 12

kuhara (fowl cholera), wiki ya 14 ndui ya kuku,

Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Shadidi

 Majogoo watenganishwe na mitetea katika wiki 7 hadi 10 ili

kuzuia uzaliano usio na mpangilio,

 Wapewe chakula cha kukuzia kuanzia wiki ya 8-15 gramu 55-

60 na kuanzia wiki ya 16 gramu 65-80 kwa wanaofugwa mfumo

huria na gram 120-125 kwa kuku kwa siku kwa wanaofugwa

mfumo wa shadidi,

 Kuku wa nyama wapatiwe chakula cha kuku wa nyama muda

wote,

 Wapatiwe maji safi ya kunywa kwa muda wote kwenye

vyombo safi,

 Kuku wachunguzwe dalili zozote za ugonjwa ili waweze kupata

tiba sahihi kutoka kwa mtalaamu wa mifugo,

 Kuku wa wiki 9-20 wanahitaji nafasi ya mita za mraba 0.15 kwa

kuku na wiki 21 au zaidi mita za mraba 0.2 kwa kuku,

 Kuwe na vyombo maalum vya kutosha kwa ajili ya chakula na

maji,

 Wafanyiwe usafi wa banda mara kwa mara ili kuzuia magonjwa

yanayotokana na uchafu

 Wakatwe midomo ili kuzuia kudonoana.

 Kuku Wanaotaga

Mahitaji ya kuku wanaotaga ni tofauti na makundi mengine.

Mambo ya kuzingatia kwa kuku wanaotaga ni pamoja na:-

1.    Banda liwe na viota vya kutagia mayai (kiota 1 kwa kuku 3-

2.   Viota viwekwe bandani mara kuku watakapofikisha umri wa

wiki 18 ili waanze kuzoea kuvitumia,

3.    Wapatiwe chakula na maji safi wakati wote kwa kutumia

vyombo maalum ambavyo ni visafi,

4.    Kuku wasiotaga waondolewe kwenye kundi.Kuku hao

huonekana wasafi na sehemu ya kutolea yai huwa ndogo na

kavu,upanga wake kichwa (comb) huwa mdogo na

mwekundu,

5.    Wapatiwe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3,

6.    Wawekewe fito au ubao mwembamba kama sehemu ya

kupumzikia na mazoezi ili kuzuia kudonoana,

7.    Mayai yakusanywe mara 4 au zaidi kwa siku ili yasidonolewe

na kuku,

8.    Kuwe na malalo makavu na yabadilishwe mara yanapochafuka,

9.    Vyombo vifanyiwe usafi kila ili kuzuia magonjwa; na                              10.Watundikiwe majani mabichi aina ya mchicha,papai,
alfaafa au majani jamii ya mikunde 
.......................................................................................
Previous Post Next Post