Sasa


Tujifunze magonjwa ya ng'ombe

Magonjwa ya ng'ombe

Magonjwa ya ng'ombe

Ndugu mfuatiliaji wa app yetu ya ufugaji na matibabu leo nataka nikuletee baadhi ya magonjwa ya ng'ombe .Tutapata kujifunza na kujadili kwa pamoja magonnjwa yanayo sumbua ng’ombe.

I. MINYOO YA NG'OMBE.

Ugonjwa wa minyoo husababisha hasara kwa mfugaji wa ng'ombe . Utafiti unaonyesha kuwa ng'ombe wengi wanaathirika na minyoo hiyo hupunguza uzalishaji. Aidha utafiti unaonyesha kuwa tatizo la minyoo kwa ng'ombe limeenea hapa nchini kwetu.

(i) AINA ZA MINYOO.

Minyoo inayoathiri ng'ombe imegawanyika katika makundi mbalimbali kama ifuatavyo;

*       Minyoo inayoishia kwenye maini ya ng'ombe (liverflukes).

*       Minyoo inayoishia kwenye mapafu (lungworms).

*       Minyoo mikubwa ya mviringo (large roundworms).

*       Minyoo midogo ya mviringo (small roundworms).



Dalili za ng'ombe mwenye ugonjwa wa minyoo.

v  Kupoteza uzito

v  Kukosa hamu ya kula

v  Kuhara

v  Kupungukiwa na damu

v  Kuwa na homa

v  Afya yake kufifia na hatimaye kufa

v  Tumbo kuwa kubwa kupita kiasi (ndama).


Namna ya kutibu.

Wanyama wapewe dawa za kutibu minyoo mara kwa mara.
Mfano:

v  NILVERM

v  PIPERAZINE

v  THIABENDAZOLE

v  OXYDOZIDENE

KUMBUKA;Haya yote yanapatikana katika maduka ya mifugo yaliyo karibu nawe


Madhara ya minyoo.

1.    Husababisha upungufu wa damu.

2.    Husababisha upungufu wa maziwa.

3.    Ng'ombe huweza kufa.


.................................................................................
Previous Post Next Post