Ufugaji kuku
Masoko
Mambo kadhaa ya msingi
yatakayomsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu
katika biashara
unayoifanya:
Kwanza kabisa jiulize kama bidhaa unayozalisha ina soko? Na kama
soko lipo:
• Lipo wapi na
hali ya miundombinu za kulifikia iko vipi ( ili afahamu gharama ya kufika
sokoni kama utaamua kuuzia sokoni).
• Bidhaa inahitajika kwa
wingi kiasi gani na wakati gani sokoni
• Soko linahitaji
bidhaa yenye sifa zipi ( ubora n.k. ili uzalishe sawa na matakwa ya soko
n.k)
• Kama wanunuzi
watakuwa na utayari kununulia unakozalishia, je unao uwezo wa
kutosheleza
mahitaji yao (ili uweze
kujipanga kukidhi mahitaji kwa kuongeza uzalishaji
au kwa kuungana na wazalishaji wengine).
• Linganisha bei
ya bidhaa sokoni na bei ya kuuzia unakozalishia (ili ujue palipo na faida
zaidi kwako baada ya kuondoa gharama za kufuata soko) Ila ukiamua
kuuzia sokoni
hakikisha unao uwezo wa kushindana na wauzaji wengine huko sokoni.
Majibu ya maswali haya ndiyo yatakayokupa msingi wa kujipanga
kiuzalishaji ili hatimaye
upate faida. Hivyo hata kabla hujaanza kuzalisha fahamu haya
yaliyotajwa hapa juu.
Kutafuta na kutumia taarifa za masoko ya sehemu tofauti
Kwa kadri utakavyokuwa unaendelea kuzalisha, mabadiliko mbali
mbali yatatokea
kuhusiana na uzalishaji wako na hata kuhusiana na soko la bidhaa
unayozalisha kwa
maana ya kuku.
Ili uendane na mabadiliko yanayotokea ni muhimu mzalishaji upate
taarifa za hali ya
soko mara kwa mara. Taarifa hizi zitakusaidia kufanya maamuzi
yatakayokuwezesha
kuendelea kupata faida.
Taarifa za masoko zinaweza kupatikna kwa wazalishaji kadhaa
kuungana na kuunda
umoja wao. Katika umoja huo wawakilishi wachache wanakuwa na
jukumu la kutafuta
taarifa za masoko ya kuku sehemu mbali mbali ambako kunaweza
kuwapa wazalishaji
tija zaidi.
Walio katika umoja huo watatumia taarifa hizo kufanya maamuzi ya
kuuza kwa faida
zaidi kwa pamoja au kwa mmojammoja kutegemeana na hali halisi.
Tags:
MBINU ZA UFUGAJI
.jpg)