MALISHO YA ASILI NA YALIYOBORESHWA YA NG'OMBE

Malisho ya Ng'ombe
Uboreshaji na usimamizi wa malisho ya asili
Chakula kikuu cha ng’ombe ni nyasi na majani jamii ya mikunde ambayo haia madhara kwa afya ya mnya
 Malisho ya Asili
Malisho haya kwa kawaida hukua haraka na kupoteza viinilishe muhimu, kwa muda mfupi
baada ya mvua. Malisho ya asili huwa na viinilishe vinavyotosheleza mahitaji ya mifugo na
wakati wa kiangazi malisho huwa duni na yasiyotosheleza. Wakati malisho yanatosheleza
ng’ombe huwa na uzito wa kuridhisha tofauti na wakati wa kiangazi ambapo ng’ombe
hupungua uzito. Malisho ya asili ya jamii ya nyasi huwa na upungufu wa viinilishe hususani
protini. Mikunde ina tabia yakutopungua viinilishe haraka ikilinganishwa na nyasi.
Malisho yaliyoboreshwa
Malisho ya asili yanaweza kuboreshwa kwa kuongeza mimea aina ya mikunde, kuongeza
nyasi bora kwenye malisho, kuongeza samadi kwenye mbuga za malisho. Malisho
yaliyoboreshwa yana uwezo wa kuwafanya wanyama wakue haraka na kufikia uzito wa
kuchinjwa mapema.
Taratibu za kuboresha malisho/ Mambo ya kuzingatia
i. Uwezo wa kuvumilia hali ya hewa na mazingira yaliyopo
ii. Yawe yenye kuvumilia magonjwa na wadudu waharibifu
iii. Yawe yasiyozidiwa nguvu na magugu
iv. Yawe yenye kustahimili kuchungwa
Inafaa maeneo ya kuchungia/kulishia yatengwe na kugawanywa katika sehemu ambazo
nyasi zitaoteshwa na kukuzwa. Hatimaye nyasi hizo zichungwe kwa nyakati tofauti ili
kuepuka uharibifu na kuhakikisha kuwa nyasi zinatosheleza vipindi vyote vya mwaka.
Utaratibu huo utasaidia pia kupunguza uwezekano wa mifugo kuambukiza magonjwa.
 Uhifadhi wa malisho
Malisho hupatikana kwa wingi wakati wa masika, na wakati huo yana ubora unaotakiwa.
Wakati wa masika, mifugo hula malisho na kusaza ambapo wakati wa kiangazi malisho
huwa haba na virutubisho hupungua ili kuwa na uhakika na upatikanaji na chakula cha
kutosha na bora wakati wote, ni muhimu kuhifadhi malisho ya ziada katika kipindi hicho.
Njia za kuhifadhi malisho
Kuna njia kuu mbili za kuhifadhi malisho nazo ni;
i. Kuyakausha (Hei)
ii. Kuyavundika (Saileji)
 Kuyakausha (Hei)
Hei ni majani makavu ambayo yanaweza kulishwa wanyama yangali shambani au kuvunwa
na kufungwa kwenye marobota kisha kuhifadhiwa kwa matumizi ya baadae

Hatua ya kutayarisha
i. Vuna majani yanapoanza kutoa maua
ii. Yaanike na yageuze majani mara moja au mara mbili kwa siku ili yakauke vizuri
iii. Ukaushaji huchukua siku tatu hadi sita kutegemea aina ya majani au hali ya hewa
iv. Majani yakiisha kauka yafunge kwenye marobota
v. Yahifadhi marobota sehemu isiyoingiza mvua au unyevu
vi. Marobota ya majani makavu yanaweza kutengenezwa kwa mashine au kwa
kutumia makasha ya mbao.
vii. Mfugaji mdogo anashauriwa kutumia makasha ya mbao kwa kutengeneza
marobota hayo.
viii. Makasha ya mbao yanaweza kutengenezwa kwa kutumia vipimo vifuatavyo,urefu
sentimita 75, upana sentimita 45 na kina sentimita 35.
ix. Majani yaliyofungwa katika marobota hutumia sehemu ndogo ya kuhifadhia na pia
hupunguza upotevu.
x. Mfugaji anaweza kukadiria kiasi cha malisho atakayotumia kulisha ng’ombe wake
kwa msimu wa kiangazi.
 Masalia ya mazao shambani
Masalia ya mazao kutoka shambani yanaweza kutumiwa ili kufidia chakula ambacho
ng’ombe amekikosa kutokana na uhaba wa majani wakati wa kiangazi. Masalia yanaweza
kuwa ya mabua ya nafaka mbalimbali kama vile mahindi, mtama, mpunga, ulezi, ngano au
uwele. Mengine ni majani ya viazi vitamu, miwa au majani ya jamii ya mikunde kama vile
maharage,kunde, njugu mawe au mbaazi.
Masalia yanaweza kutumiwa na ng’ombe moja kwa moja bila kuboreshwa. Hata hivyo
ng’ombe hawezi kula kwa wingi na hivyo inashauriwa kuyanyunyuzia molasses au magadi
ili ng’ombe aweze kula mengi zaidi.
 Maji
Maji ni muhimu katika kupoza joto la mwili kutengeneza maziwa, kusafirisha virutubisho
na kutoa uchafu mwilini kwa njia ya mkojo,kinyesi kupumua na jasho. Ng’ombe akipata
maji ya kutosha hukua vizuri, huwa mwenye afya na hutoa maziwa mengi na bora. Kiasi
cha asilimia 85 hadi 87 ya maziwa ni maji. Ng’ombe anapokosa maji hukosa hamu ya kula
na hali hiyo ikiendelea hupungukiwa maji na hupoteza uzito. Ng’ombe anaweza kupata
maji kwa njia zifuatazo;
i. Kunywa
ii. Kula vyakula vyenye maji maji
 Vyakula vya ziada
Hakikisha mifugo yako wanapata vyakula vya ziada kama vile
i. Pumba za mahindi, mtama,ngano
ii. Mashudu ya pamba au alizeti
16
iii. Madini
iv. Vitamini
Unenepeshaji wa ng’ombe wa asili kwa ajili ya soko
Umri unaofaa kumuuza ng’ombe wa asili ili kupata nyama bora ni miaka mitatu na nusu.
Katika umri huu ng’ombe wanaotegemewa kupelekwa kwenye soko kwa ajili ya
kuchinjwa ni madume, maksai na mitamba wasiofaa kuzaai. Ili kupata bei nzuri ya
ng’ombe mfugaji anatakiwa kuzingatia ubora wa mifugo yake kulingana na madaraja. Hapa
nchini ng’ombe wa nyama wanaouzwa wameainishwa katika madaraja matano ambayo ni:
i. Tanzania bora
ii. Daraja la kwanza
iii. Daraja la pili
iv. Daraja la tatu
v. Daraja la nne

..............................................................................................................................
Previous Post Next Post