UFUGAJI NG'OMBE WA KIENYEJI

 Ufugaji wa ng'ombe wa asili  
UFUGAJI NG’OMBE WA KIENYEJI

Ufugaji wa ng’ombe wa Asili hufanyika katika mashamba makubwa ya serikali, mashamba
madogo na wafugaji wadogo.
 Ng’ombe wa maziwa wa asili hufugwa kwa wingi katika
mikoa ya Kagera, Arusha, Mbeya, Manyara na Kilimanjaro. Hata hivyo, wanaweza
kupatikana pia katika mikoa ya Iringa, Dar es Salaam, Morogoro na Iringa. Ufugaji bora
wa ng’ombe wa maziwa humuongezea kipato mfugaji pamoja na kujipatia lishe itokanayo
na maziwa.
Ufugaji holela wa ng’ombe ni ule usiozingatia kanuni na misingi ya ufugaji na una madhara
makubwa.
 Madhara hayo ni pamoja na:
  •  Kupata mapato duni
  •  Uharibifu wa mazingira
  •  Ugonvi na migogoro katika jamii.
  •  Kutumia muda mwingi katika kuchunga badala ya shughuli nyingine
  •  Ni rahisi ng’ombe kushambuliwa na kueneza magonjwa
  •  Watoto hukosa elimu kwa kuwa hujihusisha na kuchunga ng’ombe
  •  Malisho duni kutokana na kufunga ng’ombe kuliko uwezo wa nyanda husika
  •  Ufugaji huu hauzingatii ubora bali wingi wa mifugo.
 Sifa za ng’ombe wa asili
i. Wana uwezo wa kustahimili magonjwa
ii. Hustahimili muda mrefu bila malisho yakutosha
iii. Wanaweza kutembea mwendo mrefu kutafuta maji na malisho
iv. Nyama na maziwa yao yana ladha nzuri
v. Maziwa yao yana mafuta mengi kuliko ya ng’ombe wa kisasa
......................................................................................................................

Previous Post Next Post