FAHAMU AINA YA CHAKULA CHA KUKU NA CHANJO ZAKE

AINA ZA CHAKULA NA MFUMO WA KULISHA:
KUKU WA NYAMA(broilers)
Broiler starter(wiki 3 za kanza)
Broiler finisher hadi kuuza.
UTARATIBU WA CHANJO
Umri wa siku 7:  Newcastle(kideri)
Umri wa siku14 :  Gumboro
Umri wa siku 21:  New castle(kideri)                                                                                                              
 Umri wa siku 28:Gumboro 
Sifa za banda bora la kuku..
1. Liwe limejengwa mahali palipokingwa na upepo mkali.
2. Liwe na mwanga wa kutosha.
3. Madirisha yaruhusu hewa safi kuingia na chafu kutoka (Cross Ventilation).
4. Sakafu isiruhusu maji kutuama wala maeneo yanayozunguka banda.
5. Paa lisiruhusu mvua kuingia.
6. Banda liwe linasafishika kwa urahisi na kuta imara.
7. Banda liwe na nafasi ya kutosha kwa ajili ya kuku, vyombo vya maji na chakula,
NAFASI YA KUKU WA NYAMA (STOKING RATE)
Mita za mraba (m2): 4m2=kuku 50-100
MATATIZO YALETWAYO NA UPUNGUFU WA VITAMINI MWILINI(2)

VITAMINID                                                                                                                   
Husaidia madini aina ya calcium na phosphorous kuchukuliwa na mwili ili kuimarisha mifupa na kutengeneza ganda la yai la kuku. Jua husaidia mwili wa kuku kutengeneza vitamini D.
Dalili za Upungufu wa Vitamini D Mwilini

Rickets: Mifupa huwa laini(soft), hupinda, magoti huvimba, na midomo huwa laini. Hii hutokana na madini aina ya calcium na phosphorous kutojengeka kwenye mifupa.
Kukua polepole.
Uanguaji hafifu wa mayai.
VITAMINIE
Dalili za Upungufu wa Vitamini E Mwilini

Ugonjwa uitwao "crazy chick" au "nutritional encephalomalacia" ambapo ubongo wa kuku huwa laini na kuathiri mishipa ya fahamu.                                                                                                                                                    
  Dalili zake ni
                  -Shingo hupinda
                   -Kifaranga huanguka kifudifudi
                   -Kichaa
VITAMINI K
Husaidia kuzuia kuvuja damu. Ikikosekana mwilini mishipa ya damu hupasuka na kusababisha damu kuvuja. Vitamini hii hupatikana katika alfalfa, samaki (fish meal) na nyama.
VITAMINI B1 (THIAMIN)
Huleta hamu ya kula.
Upungufu hufanya kichwa kurudi nyuma (Head retraction)

 Siyo rahisi kupata upungufu wa vitamini B1 mwilini kwa kuwa vyakula vingi vina vitamini hii.Hupatikana katika nafaka, alfalfa na mafuta (oil).                                  
NAMNA YA KUZUIYA MAGONJWA
Weka dawa ya kuua wadudu kwenye chimbo mlangoni ili watu waikanyage
(disinifectant +maji)
Punguza mwanga kwa kuku wanaokua
Wiki ya kwanza tumia dawa aina ya ANTIBIOTIC na VITAMIN kwenye maji
hapa ni vizuri ukapata ushauri

...........................................................................................................................................
Previous Post Next Post