BANDA BORA LA NG'OMBE WA MAZIWA

banda la ng'ombe wa maziwaBANDA/ZIZI BORA LA NG’OMBE WA MAZIWA.
Band alijengwe sehemu ya mwinuko mbali kidogo na makazi ya watu na liwe na sifa zifuatazo:-


  • Uwezo wa kumkinga ng’ombe dhidi ya mvua, upepo, jua kali na baridi.
  • Kuta imara zenye matunda au madirisha kwa ajili ya kuingiza hewa na mwanga wa kutosha,
  • Sakafu yenye mwinuko upande mmoja ili isiruhusu maji na uchafu kutuama.
  • Lijengwe katika hali ya kuruhusu kufanyiwa usafi kwa urahisi kila siku, na sakafu ngumu ya zege au udongo ulioshindiliwa na kuweka malalo.
  • Paa lisilovuja na
  • Aidha kwa wafugaji wanaofuga katika ufugaji huria ambako mazizi hutumika, inashauriwa  kuzingatia yafuatayo:-
  • Zizi likae mahali pa mwinuko pasiporuhusu maji kutuama.
  • Zizi liweze kukinga mifugo dhidi ya wezi na wanyama hatari.
  • Ukubwa wa zizi uzingatie idadi na umri wa mifugo ng’ombe watengwe kulingana na umri wao.
  • Zizi lifanyiwe usafi  mara kwa mara na
  • Liwe na sehemu ya kukamulia (kwa ng’ombe wa maziwa), stoo ya vyakula, sehemu ya kutolea huduma za kinga na tiba, eneo la kulishia na maji ya kunywa.


ZIZI BORA
Zizi lijengwe sehemu ya mwinuko isiyoruhusu maji kutuama mbali kidogo na makazi ya watu na liwe na sifa zifuatazo:-

  • Liweze kuhakikisha usalama wa ng’ombe.
  • Ukubwa wa zizi uzingatie idadi ya mifugo.
  • Liwe na sakafu ya udongo ulioshindiliwa vizuri na kufanyiwa usafi  mara kwa mara
  • Zizi la ndama liwe na paa ma
  • Lijengwe kwa vifaa madhubuti na visivyoharibu ngozi.


UCHAGUZI WA KOO NA AINA YA NG’OMBE WA KUFUGA
Kwa ufugaji wenye tija, mfugaji anashauriwa kuchagua koo na aina ya ng’ombe kwa kuzingatia malengo ya ufugaji (nyama au maziwa).

NG’OMBE WA NYAMA
Ng’ombe wanaofaa kufugwa kwa ajili ya uzalishaji nyama ni wale wanaokua kwa haraka na kuweka misuli mikubwa iliyojengeka vizuri.  Baadhi ya koo zenye sifa hizo ni pamoja na Boran, Mpwapwa (nyama na maziwa), Charolais, Aberdeen Angus, pamoja na chotara wao.  Hata hivyo, nchini Tanzania ng’ombe aina ya Zebu (mfano Ufipa,Gofo, Masai, Sukuma, Tarime, Iringa red), Sanga (Ankole) na chotara wao ndio hutumika kama ng’ombe.
................................................................................................................................
Previous Post Next Post