ULINZI WA VIUMBE HAI / BIOSECURITY

*BIO SECURITY* 

👆Bio👉Viumbe hai 
👆Security👉Usalama 

Kwa mjumuisho, Biosecurity..ni *viumbe hai salama* 

Yaani jumla ya mambo yote yatakayo fanyika kukinga magonjwa yasiingie kwenye shamba la kuku. 

 *UGONJWA KUINGIA SHAMBANI UNATEGEMEA YAFUATAYO* 

👉Port of entry/njia ya kuingia 
👉Resevoir host/Anaetunza vimelea bila kuumwa 
👉Succeptible host/ mnyama atakae ugua 
👉Port of exit/Njia ya kutokea 

👆Port of entry/uingiaji 
Hii ni mianya yote ambayo ugonjwa unaweza kuingia shambani, mfano 

👉Wanunuzi wa kuku 
👉Vifaa vya kusafirishia bidhaa kuja au kutoka shambani 
👉Wataalamu au madaktari 
👉Watu wasio na ulazima kuingia bandani 
👉Mavazi yasiyo rasmi 
👉Ndege, Panya, vyakula visivyo safi 

👆Hivyo ni baadhi ya vyanzo ambavyo huweza kuleta ugonjwa kuingia shambani 

 *SULUHU* 
👉Uwe na mavazi maalaumu ya kuingilia bandani 
👉Wageni wasio na ulazima wasiingie bandani (waishie nje ya banda) 
👉Madaktari wanaotembelea mradi, wawe na mavazi maalumu ya kujikinga, wasiwe wametoka kwenye shamba lenye ugonjwa, na akifika aanze kupitia kuku ambao hawaumwi na wale wanao umwa wawe wamwisho kabisa( zingatia). 

👉Wanunuzi wakija, sio wote waingie shambani, kumbuka hawa hutembelea mashamba mengi hivo huwa wasababishi wazuri wa kubeba ugonjwa kutoka point A-B-C ( *Zuia wasifike na Kuku kutoka shamba jingine kuja nao kwenye shamba lako* ) 

👉Ziwepo dawa za kunawa mikono (sanitizer), na Dawa za kukanyaga kabla ya kuingia bandani 

👉Kuwe na utaratibu maalumu wa kuteketeza mizoga ya kuku waliokufa....hayo ni baadhi. 

👆Resevoir Host(mbebe vimelea asie ugua). 
👉Huyu ni kiumbe yoyote anae weza kubeba vimelea vya ugonjwa ila yeye asiugue 

Mfn. 
Ndege pori-Mafua 

Kuchanganya makundi ya ndege tofauti mfn-Bata na kuku( kitaalamu hairuhusiwi) 

Panya-Salmonella 

Viroboto, utitiri, mbu nk 

 *Hawa kwa namna yoyote wanatakiwa kudhibitiwa kuto ingia bandani...kupunguza kasi ya maambukizi.* 

👆Succeptible host( Kuku mwenyewe) 

👉Huyu ni kiumbe ambae ataugua ugonjwa, au ataonesha dalili za maambukizi, mara baada ya vimelea kuingia shambani utapita muda ( incubation period) kisha vimelea watakua wamezaliana kiasi cha kupelekea infection na hatimae ugonjwa 

🤛 *Hivo hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa ili kudhibiti vyanzo vya ugonjwa visiingie.* 

👆Port of exit/Utokaji wa ugonjwa 
👉Kwa namna gani ugonjwa unaweza kutoka shambani, 

👆Mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa,
👉Mayai yaliyotoka kwa kuku anaeumwa 
👉Vifaranga waliotoka kwa kuku anaeumwa 
👉Kuku wanao uzwa kwenda mahala pengine. 

Hivo nimihimu sana mfugaji ukawa unafahamu Chanzo cha kuku wako ili kuepuka matatizo yanayo weza kuzuilika 
Previous Post Next Post