Mifugo
Mifugo au Wanyama wa kufugwa ni wanyama wanaopatikana kutokana na ufugaji wa kibinadamu.
Wako tofauti na wanyamapori baada ya na mchakato mrefu ambako wanyama wa pori ama walijiunga na binadamu au walishikwa nao na watoto wao kuteuliwa kutokana na tabia zilizopendelewa na wafugaji wao. Tabia hizo ni pamoja na upole na uwezo wa kupatana na binadamu, uwezo wa kuzalisha kiasi fulani cha nyama au maziwa, uwezo wa kustawi kwa chakula fulani au katika mazingira mbalimbali.
Katika mchakato wa vizazi vingi tabia zilizolengwa ziliimarishwa katika spishi zinazofugwa.
Uteuzi huu umesababisha tofauti za kimaumbile na tofauti za tabia baina ya wanyama wa kufugwa na wanyamapori wa spishi ileile. Tofauti hizi zinaonekana katika rangi, ukubwa wa mwili, uwezo wa kuwasiliana na binadamu na mengine.
Wako tofauti na wanyamapori baada ya na mchakato mrefu ambako wanyama wa pori ama walijiunga na binadamu au walishikwa nao na watoto wao kuteuliwa kutokana na tabia zilizopendelewa na wafugaji wao. Tabia hizo ni pamoja na upole na uwezo wa kupatana na binadamu, uwezo wa kuzalisha kiasi fulani cha nyama au maziwa, uwezo wa kustawi kwa chakula fulani au katika mazingira mbalimbali.
Katika mchakato wa vizazi vingi tabia zilizolengwa ziliimarishwa katika spishi zinazofugwa.
Uteuzi huu umesababisha tofauti za kimaumbile na tofauti za tabia baina ya wanyama wa kufugwa na wanyamapori wa spishi ileile. Tofauti hizi zinaonekana katika rangi, ukubwa wa mwili, uwezo wa kuwasiliana na binadamu na mengine.
Asili katika wanyama waliotafuta mazingira ya kibinadamu
Inaonekana ya kwamba kulikuwa pia na wanyama wengine wa porini waliofuata binadamu kwa sababu waliona faida kukaa karibu nao kama vile paka (aliyefuata panya waliokula mavuno ya wakulima wa kwanza).
Vilevile asili ya kuku ni kuku mwekundu wa porini wa Indonesia (red junglefowl) aliyetafuta takataka kwenye makazi ya watu, akawazoea na kutumiwa nao kama chanzo cha nyama na mayai.
Tags:
MBINU ZA UFUGAJI