HOMA YA MATUMBO KWA KUKU (Fowl Typhoid):

Fowl Typhoid
HOMA YA MATUMBO KWA KUKU  (Fowl Typhoid):
                     Ugonjwa huu husababishwa na Bakteria na huwapata kuku wa umri wote. Ugonjwa huu huambukizwa kutoka kwa kuku wagonjwa kwenda kwa kuku wasio wagonjwa, kupitia kwenye mayai, chakula chenye kinyesi cha kuku wenye ugonjwa pia watu iwapo watabeba vimelea na kuja navyo kwenye banda.
JINSI UNAVYOAMBUKIZA
                 Kuku asiye mgonjwa kula vimelea vya ugonjwa kupitia kinyesi cha kuku mgonjwa kwenye chakula.
Kuku mgonjwa huweza kurithisha vifaranga wake kupitia mayai aliyotaga.
Watu na vyombo vya usafiri wanaweza kuhamisha ugonjwa kutoka sehemu hadi sehemu.
Vyakula vya kuku kutoka sehemu yenye ugonjwa kwenda kusiko na ugonjwa.
Mizoga ya kuku yenye ugonjwa ikipelekwa sehemu isiyo na ugonjwa.
DALILI
Homa kali.
Manyoya husimama.
Kinyesi kuonekana kuganda sehemu ya nyuma.
Kukosa hamu ya kula.
Kuku kudhoofika.
Kiwango cha utagaji hushuka.
KINGA
Tenganisha vifaranga na kuku wakubwa.
Kuku wagonjwa watengwe na kupewa tiba ya antibiotic.
Zingatia usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji.
MATIBABU
Dawa aina ya Oxytetracycline (OTC) au Salfa ambayo huchanganywa kwenye maji na kupewa
kuku kwa siku 5 hadi 7.
....................................................................................................................
Previous Post Next Post