Vifaa
na Vyombo Muhimu
Mfugaji anashauriwa
kutumia vifaa na vyombo maalum ili kurahisisha na
kuboresha utunzaji wa
makundi mbalimbali ya kuku. Vifaa na vyombo
vinavyohitajika kwa
ajili ya kuwekea chakula na maji, kutagia mayai na
kupumzika vinapatikana kwenye
maduka ya pembejeo za mifugo. Aidha,
mfugaji anaweza
kutengeneza mwenyewe kwa kutumia malighafi zilizopo
kwenye mazingira yake.
Uchaguzi wa Kuku Bora wa Kufuga
Kuku wa Asili
Aina za kuku wa asili
wanaopatikana nchini Tanzania ni pamoja na Kuchi
(Kuza), pori
(Kishingo), Njachama, Kinyavu, Mbuni na Tongwe nchini Msumbiji.
Mfugaji anaweza
kuongeza uzalishaji kwa kuchagua kuku mwenye sifa
zifuatazo:-
v Uwezo
wa kutaga mayai mengi (kati ya 15-200 katika mzunguko
mmoja wa utagaji
v Uwezo wa kuatamia na kuangua
vifaranga wengi,
v Uwezo wa kustahimili
magonjwa
v
Umbo kubwa na kukua haraka.
Tags:
KUKU