USUGU WA DAWA KWA KUKU

HELOW WAFUGAJI TWENDE SAMBAMBA HAPA 

Kunakitu kinaitwa usugu wa madawa kwa mifugo na binadamu kwa kingereza DRUG RESISTANCE 

Kwa mujibu wa tafiti kadha wa kadha hili tatizo limekua likiongezeka siku kwa siku na inasemekena bidhaa zitokanazo na kuku zimechangia kwa sehemu kubwa katika swala hili 

LINATOKEAJE 

Kila dawa anayopewa mnyama huwa ina muda wa kukaa na kupotea kwenye nyama au mayai/ withdrawal period 

Kila dawa unayoitumia imeandikwa utumie nyama au mayai baada ya muda gani nivema kuzingatia saana kwani madhara yake hayapo kwa kuku tu bali huhamia hadi kwa binadamu 

Tuelewe kuna baadhi ya dawa kwa mfano zinzoua bakteria zikitumika zinabaki mwilini kwa muda tofauti..kama utatumia bidhaa yanye kiwango kikubwa chenye dawa...madhara yake nikwamba vimelea wa magonjwa husika huwa sugu na kutosikia dawa na hii inakuja kupelekea hatakama utatumia dawa ya aina hiyo haitafanya kazi tena utalazimika kutumia dawa nyingine kwahiyo garama inapanda maradufu 

Piaa kutumia dawa isiyo sahihi kwa ugonjwa hukomaza vimelea vya magonjwa na kusababisha kutosikia dawa kwa muda mrefu 

SHIDA IPO HAPA 

Hutakiwi kuanza kutumia dawa zenye dozi kubwa mapema kabla ya kuanza na dawa zenye dozi ndogo..hiii inabidi ujue na utekeleze hasa kwa kuwahi kuwachunguza kuku wako mapema kugundua kama wanaumwa mapema na kuwaanzishia dozi

Hii ndo husababisha kwa mfano..mmoja Fluban ifanye kazi na kwa mwingine  isifanye kazi...kwa mfano mapema kabisa kuku wamepata mafua usikimbilie dozi kubwa kama Enrovet au dawa kali za mafua.. Madhara yake kama itashindwa kutibu itakuletea ugumu kupata mbadala wa dawa kutibu magonjwa 

Pia kuna swala la kuchanganya dawa bila kujua kama zinafaa kuchanganywa au laa hii pia imepelekea kuku na bidhaa za mayai kubaki na masalia makubwa ya dawa na usugu umeongezeka maradufu...kumbuka kuna dawa nyingine ukichanganya na nyingine huzuia utendaji kazi wa mojawapo hili niswala pana na linahitaji mtaalamu au Daktari mbobezi akuthibitishie ndipo uchanganye 

Usitumie dawa marakwamara bila sababu za msingi...inashangaza kuona mtu anaamua kuanza kutumia dawa bila kuku kuumwa unafanya wawesugu...japo kama itafanyika katika utaalamu na dozi ndogo hupelekea kuweka kama kinga flani...ila iwe chini ya usimamizi wa daktari wa mifugo wa upande huo. 

Chakuzingatia hapa ndugu mfugaji jitahidi sana USAFI WA BANDA...na banda lako likae katika Ubora sahihi ya ujenzi hasa unaoruhusu mzunguko wa hewa bandani 
Previous Post Next Post