UFUGAJI WA KUKU

NASAHA ZA UFUGAJI 

Kufuga kuku kunahitaji uelewa wa vitu vingi sana ili uweze kwenda katika mtazamo wa kukupa, faida 

Ufugaji wa kuku ni zaidi ya kuwa na pesa ya mtaji kwani..unaweza ukawa na mtaji ukaingia kufanya mradi wa kuku ila kama hutakua na mbinu sahihi za kitaalamu za ufugaji unaweza pata maendeleo hasi 

Ufugaji wa kuku unahitaji utulivu wa mawazo, kufanya utafiti na kujua kwa kina changamoto zilizopo katika nyanja hii ya kuku 

Mfugaji unatakiwa kujua mahitaji yote muhimu yanayo mfanya kuku akue vizuri na kumtimizia haki zake za msingi kama vile 
=Chakula na maji 
=Nyumba sahihi ya kuishi 
=Kuwa huru dhidi ya magonjwa 
=Kuku asiwe na msongo wa mawazo 
=Kuku awe katika fikra zako kama sehemu ya maisha yako 
=Joto,hewa safi na mwanga bandani 

Pia kuku kama mradi unatakiwa kujua kwa kina juu ya soko na vipi utapambana na soko kwa kuzingatia kubadilika kwa gharama za uendeshaji 

Kuku kama mradi unakuhitaji kufahamu wataalamu ambao unaamini watakusaidia pale unapopata changamoto na usitatue changamoto yako kwa kuiga fulani alifanya nini hasa kwenye magonjwa 



Kuku ili alete faida inabidi uhakikishe umepunguza magonjwa kwa kiasi kikubwa hivyo gharama za dawa zisiwe nyingi,,,,hili ni kwa kuhakikisha usafi wa banda na mzunguko mzuri wa hewa 

Kuku kama mradi unahitaji uangalizi wa karibu na Mara kwa Mara...muweke mhudumia kuku atakae wapenda kuku na kuwachunguza mabadiliko yao marakwamara na kuyatatua 

Kwa afya bora ya watumiaji mfugaji...epuka kuuza bidhaa za kuku ambazo muda wa kukaa baada ya kutumia madawa haujaisha huu ni utu na nidhamu ya biashara 

Pia ili kuendana na soko mgugaji jitahidi kuzalisha bidhaa bora ambayo itakua na mvuto sokoni...mayai au nyama vikidhi viwango 

Kuku mradi pia unahitaji moyo wa uvumilivu na kutokata tamaa...uwe mjasiria Mali atakae chukua changamoto na imsimamishe iwe kama fursa ya kujifunza na kuanza upya kwa usahihi 

Kama wafugaji wa kuku huko mbeleni tutapaswa kuwa na UMOJA ambao utatusimamia kudai haki zetu...hasa pale SOKO linapo kua linashuka kukinzana na gharama za uendeshaji....ikumbukwe wanunuzi huja na msimamo wa bei gani wanunue kuku kwetu...hivyo UMOJA wetu unaweza kutusaidia kuwa na SAUTI ya pamoja juu ya masoko 


Niseme tu binafsi GREYSON KAHISE nimejitoa kuwapa elimu wafugaji kwa kadri nitakavo weza naamini katika mafunzo ninayo yatoa kipo utakachojifunza pia kumfunza hata nduguyako....nawapenda nawatakia mafanikio MAKUBWA 

ZINGATIA...kuku haufugi pekeako kwahiyo uwe makini kwa maana ya kuangalia UELEKEO wa soko ili kuepuka hasara zinazoweza kukimbilika 
Previous Post Next Post