MINYOO KWA KUKU

MAKALA KUHUSU MINYOO KWA KUKU 

Minyoo ni viumbe hai ambao huishi kwa kutegemea uwepo wa kiumbe mwingine kwa malazi na chakula 

Kwa kuku minyoo ipo ya aina nyingi, ipo ile ya duara, ipo ile inayokua mirefu sana ambayo ikiwapata kuku kupotea huchukua muda mrefu 

CHANZO CHA MINYOO 

Kuku kula chakula kichafu hasa kilicho changanyika na kinyesi...hapa hasa kama unachanganya kuku wakubwa na wadogo madhara huwa endelevu bandani usipokinga 

Kuku wanao zunguka nje, kunywa maji yaliyotuama au maji yaliyokaa kwa muda mrefu pia kuparua mabaki yenye mazalia au mayai ya minyoo 

Kwa kawaida minyoo huwa na mzunguko wao kunzia YAI, LAVA, PUPA ,NA MNYOO mnyoo mkubwa...hivyo minyoo ikiingia kwa kuku huvhukua muda wa wiki zaidi ya mbili kukua kufikia mnyoo kamili 

Kuku akishapata minyoo wakubwa...hapa ndipo tatizo huanzia kwani mahai hutagwa kwa wingi na hutolewa kwa njia ya kinyesi na kuwafikia kuku wengine hivyo kama hatua za maksudi hazitachukuliwa ndani ya muda wa wiki 4 tangu minyoo kuingia bandani asilimia kubwa ya kuku watakua na minyoo 

KUZUIA 

Hakikisha mazingira yako ni salama na safi muda wote yasiyo na maji yenye kutuama kwa wala matope yanayo kuwepo kwa muda wote kuzunguka mahali kuku wanapoishi 

TIBA 

Kitaalamu zipo dawa nyingi za minyoo ambazo kwa ratiba iliyo zoeleka hutakiwa kutolewa na kurudiwa kila baada ya miezi mitatu 

Tatizo limekuja ni upi wakati sahihi wa kuanza dozi ya minyoo...SIJAFANYA UTAFITI....ila kwa kuuliza madaktari bobezi wa kuku wanashauri dawa za awali za minyoo zitolewe baada ya miezi miwili 

INASHAURIWA KWA SEHEMU ZENYE MAJI YASIYO SALAMA SANA 

Na mfumo wa utoaji dawa za mjnyoo kwa Mara ya kwanza unatakiwa uwe wa kurudia kila baada ya wiki 2 rudia Mara tatu 

KWA NINI IRUDIWE UNAPOANZA DOZI 

Dawa za minyoo hishambulia hatua mbili za ukuaji wa minyoo..ambazo ni minyoo wakubwa na wale wanaofuata kwa ukubwa ilaa haziathiri hatua za mayai na LAVA...hivyo ukiwapa dawa kwa kurudia kila baada ya wiki mbili  Mara  3 mfululizo hii itapelekea hata yale mayai yatakua yamegeuka na kuwa minyoo wakubwa hivyo dawa itawaua na kupunguza tatizo kwa 75-85% 

Ila ukiwa unasubiri kuwapa kila baada ya miezi mitatu bila kufanya hizo hatua nilizolekeza utakua unapunguza idadi ya minyoo na wakati mwingine minyoo itazidi na haitasikia dawa 

Zipo dawa aina nyingi za minyoo kama Ant worms ...Piperezine...Albendazole ...zipo nyingi sana madukani 



KWA URAHISI 

Awamu ya kwanza ya kuwapa dawa 

Baada ya miezi miwili....dozi siku 1-2 

Rudia baada ya wiki 2 dozi siku 1-2 

Rudia baada ya wiki 2 dozi siku 1-2 

Ukimaliza hapo sasa wape dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu kuku wako watakua salama na huru dhidi ya minyoo 

ZINGATIA 

▶maji safi 
▶chakula safi 
▶banda safi 
▶na fuata ratiba sahihi ya dawa hasa kila baada ya miezi mitatu zingatia usipitishe na uzipuuze 
Previous Post Next Post