CHAKULA MBADALA CHA KUKU

CHAKULA MBADALA
UOTESHAJI WA MAJANI HYDROPONICS FODDER 

Hydroponics ni majani au mboga mboga zinazooteshwa kwa muda mfupi...hapa naongelea majani au nafaka za kulishia mifugo 

HATUA ZA KUFUATA 

Unachukua aina yoyote ya nafaka mfano. Mtama, mahindi au uwele 

Unaosha nafaka utakayo amua kutumia kwa jiki kama inapatikana 

Baada ya hapoo unayatoa kwenye maji uliyokuwa unasafisha hizoo nafaka 

Unaloweka nafaka uliyoisafisha kwa maji safi kwa muda wa masaa 12 

Baada ya masaa 12 nafaka yako itakuwa imeshapata maji ya kutosha 

Unaziweka nafaka zako kwenye chombo ambacho kinapatikana sana sana wanatumia trey maalum za kuwekea ambazo zipo kama sahani au sinia 

unazifunika kwa nylon yoyote lakini sana sana wengi wanatumia gazeti au nylon nyeusi 

Unaziweka kwenye chumba ambacho hakipitishi mwanga kwa muda wa masaa 48 

Baada ya masaa 48 ukienda kufunua utakuta nafaka uliyochagua imeota nyuzi nyuzi nyeupe 

utatakiwa utoe trey za hiyo nafaka uliyochagua na kuweka sehemu iliyotengenezwa rasmi kama kichanja 

 tray zina beba gram 200-500...na kuendelea inategemeana na ukubwa 

Utatakiwa uwe unamwagilia maji kila maraa ziwe na unyevu 

Baada ya siku nne kuanzia ile siku uliyoweka kwenye kichanja utatakiwa uwape kuku wako kwasababu itakuwa tayari 

 Kwa ajili ya matumizi na baada ya siku saba unaweza kuwapa wanyama wengine kama sungura, ng'ombe, mbuzi, nguruwe 

Majani haya huweza kupunguza kwa kiasi matumizi ya chakula pia huwa ni muhimu kwa kuongeza vitamin kwa kuku na kupelekea afya bora. 


NB HAKIKISHA TREY ZAKO ZIMEOSHWA NA KUFANYIWA DISINFECTION/OSHA KWA MAJI YALIYO CHEMKA 

Kuzuia Moulds na Fangasi 
Previous Post Next Post