MABANDA BORA YA KUKU
Ujenzi wa mabanda bora ya kuku ni miongoni mwa mambo ya msingi kabisa katika ufugaji bora wa kuku wawe ni wa asili au wale walioboreshwa. Hata hivyo si kila mtindo wa ujenzi unafaa, kwahiyo ujenzi huo ni lazima uzingatie mahitaji halisi ili ufugaji huo uweze kutoa matokeo bora yanayotarajiwa na mfugaji.
Mambo muhimu katika ujenzi wa banda la kuku ni;
1. Liingize hewa safi wakati wote.
2. Liwe kavu daima.
3. Liwe nafasi ya kutosha.
4. Liwe la gharama nafuu lakini la kudumu.
5. Lizuie kuingia wanyama na wadudu hatari kwa kuku.
6. Liwe na nafasi ya kuweka vyombo vya chakula na maji.
7. Lizuie upepo wakati wa baridi kali.
HEWA NA MWANGA:
Hewa ni muhimu kwa kila
kiumbe, hivyo banda la kuku ni lazima liingize hewa safi na kutoa ile
chafu na liweze kuingiza mwanga wa kutosha.
1. Kwa kifupi ni kwamba madirisha ya banda ni lazima yawe makubwa na ya kutosha ili yaingize hewa safi na kutoa ile chafu.
2. Ni vema madirisha haya yawe juu kiasi cha meta moja (1) kutoka chini ili hewa ipite juu ya vichwa vya kuku.
3. Hewa
safi siyo upepo, hivyo jaribu kuzuia upepo mkali kuingia ndani ya banda
la kuku ama sivyo kuku wataugua ugonjwa wa mafua na niumonia na
vifaranga vinaweza kufa kwa ugonjwa wa baridi.
4. Jenga Banda
lako kwa kukinga upepo unakotokea na kupanda miti kuzunguka banda hilo
la kuku ili kupunguza kasi ya upepo na kuweka kivuli dhidi ya jua kali
na joto.
UKAVU NA USAFI WA NDANI:
Kwa vile kuku si ndege wa majini kama bata , ni jambo la busara kuhakikisha kuwa mahali anapoishi hapana unyevunyevu.
§ Banda la kuku lijengwe mahali palipoinuka ili kuzuia maji ya mvua yasiingie.
§ Wajengee
kuku uchaga wa kulalia kwa kuweka viguzo vyenye urefu wa meta moja na
kutandika miti juu yake ili usiku walale hapo, kuliko kuwalaza ardhini
au sakafuni.
§ Ukavu
wa banda ni muhimu sana hasa kwa vifaranga na kuku wanaotaga. Ndani ya
banda lenye unyevu mayai kuchafuka sana hata wakati mwingine huoza kwa
urahisi na jitihada zako zitakuwa ni bure.
§ Sakafu
ya banda ni vizuri ikawa ya zege lakini kutokana na uhaba wa fedha
sakafu inaweza kutengenezwa kwa mabanzi (mabanda yaliyoinuliwa) au
udongo mgumu na au mchanga ambao utafunikwa kwa mabaki ya taka za mpunga
na yale ya mbao.
§ Ili kuepuka unyevunyevu ni vyema eneo/mahali pla kujenga banda pawe pameinuka na penye kupitisha hewa ya kutosha.
PAA LA BANDA:
Paa la banda liwe madhubuti ili kuzuia maji ya mvua kuingia hasa wakati wa masika. Sakafu ya banda iwe juu zaidi ya usawa wa nje.
Paa linaweza kuezekwa kwa mabaki ya vipande vya bati , madebe na kama
ikishindikana tumia nyasi zinazofaa kwa ajili ya kuezeka nyumba katika
eneo hilo.
NAFASI YA KUFANYA KAZI:
Banda la kuku lisiwe na nguzo au mbao nyingi sana
ndani kiasi cha kumfanya mhudumiaji wa kuku ashindwe kufanya kazi zake.
Hali hiyo itamfanya apoteze muda mwingi katika kuzizunguka nguzo hizo,
hasa wakati wa kuokota mayai au kufanya usafi.
VIFAA:
Unapotaka kujenga banda la kuku kwanza kabisa tayarisha vifaa vinavyotakiwa. Vitu kama miti au nyasi, nyavu au fito, misumari au kamba ni muhimu kuviandaa mapema.
Pili ni lazima uwe na plani/ramani kamili ya banda
hilo. Kwa wastani kila kuku anahitaji nafasi ya Meta za eneo la 0.11
hadi 0.22 (futi 1 hadi 2 za eneo.) kutegemeana na umri wa kuku.
UJENZI RAHISI:
Kuku wafugwao hatimaye ni lazima wafidie gharama za
Ujenzi wa mabanda na chakula. Gharama zikiwa kubwa sana huenda ukaifanya
shughuli ya ufugaji isiwe na faida hata kidogo hali hiyo itamfanya
mfugaji aone ufugaji hauna maana yoyote kwake. Lakini ukijenga banda
lako kwa kutumia vifaa vinavyopatikana kwa urahisi utaongeza faida zaidi
kwakuwa umepunguza gharama za uendeshaji wa mradi.
VIPIMO:
Banda la
kuku linatakiwa liwe na Meta 15 hadi meta 22 za eneo yaani Meta 3 hadi
4.5 za upana kwa meta 5 za urefu. Banda hili linaweza kutunza kuku 100
wakubwa kwa wakati mmoja.
HITIMISHO;
· Ujenzi wa mabanda unasisitizwa katika kuboresha ufugaji wa kuku wa asili ili;
· Kuongeza
uzalishaji na kupunguza vifo vya vifaranga kwa majanga mbalimbali kama
vicheche ,mwewe, mapaka, mbwa na wizi wa kuku wanaozurura holela.
· Vile
vile inatarajiwa kwamba kuku wanaozuiliwa kwenye banda na kuwekewa
chakula mchanganyiko wataongeza uzalishaji kwa kiasi kikubwa.
Mambo muhimu katika ujenzi wa banda la kuku ni;
1. Liingize hewa safi wakati wote.
2. Liwe kavu daima.
3. Liwe nafasi ya kutosha.
4. Liwe la gharama nafuu lakini la kudumu.
5. Lizuie kuingia wanyama na wadudu hatari kwa kuku.
6. Liwe na nafasi ya kuweka vyombo vya chakula na maji.
7. Lizuie upepo wakati wa baridi kali.
HEWA NA MWANGA:
Hewa ni muhimu kwa kila
kiumbe, hivyo banda la kuku ni lazima liingize hewa safi na kutoa ile
chafu na liweze kuingiza mwanga wa kutosha.
1. Kwa kifupi ni kwamba madirisha ya banda ni lazima yawe makubwa na ya kutosha ili yaingize hewa safi na kutoa ile chafu.
2. Ni vema madirisha haya yawe juu kiasi cha meta moja (1) kutoka chini ili hewa ipite juu ya vichwa vya kuku.
3. Hewa
safi siyo upepo, hivyo jaribu kuzuia upepo mkali kuingia ndani ya banda
la kuku ama sivyo kuku wataugua ugonjwa wa mafua na niumonia na
vifaranga vinaweza kufa kwa ugonjwa wa baridi.
4. Jenga Banda
lako kwa kukinga upepo unakotokea na kupanda miti kuzunguka banda hilo
la kuku ili kupunguza kasi ya upepo na kuweka kivuli dhidi ya jua kali
na joto.
UKAVU NA USAFI WA NDANI:
Kwa vile kuku si ndege wa majini kama bata , ni jambo la busara kuhakikisha kuwa mahali anapoishi hapana unyevunyevu.
§ Banda la kuku lijengwe mahali palipoinuka ili kuzuia maji ya mvua yasiingie.
§ Wajengee
kuku uchaga wa kulalia kwa kuweka viguzo vyenye urefu wa meta moja na
kutandika miti juu yake ili usiku walale hapo, kuliko kuwalaza ardhini
au sakafuni.
§ Ukavu
wa banda ni muhimu sana hasa kwa vifaranga na kuku wanaotaga. Ndani ya
banda lenye unyevu mayai kuchafuka sana hata wakati mwingine huoza kwa
urahisi na jitihada zako zitakuwa ni bure.
§ Sakafu
ya banda ni vizuri ikawa ya zege lakini kutokana na uhaba wa fedha
sakafu inaweza kutengenezwa kwa mabanzi (mabanda yaliyoinuliwa) au
udongo mgumu na au mchanga ambao utafunikwa kwa mabaki ya taka za mpunga
na yale ya mbao.
§ Ili kuepuka unyevunyevu ni vyema eneo/mahali pla kujenga banda pawe pameinuka na penye kupitisha hewa ya kutosha.
PAA LA BANDA:
Paa la banda liwe madhubuti ili kuzuia maji ya mvua kuingia hasa wakati wa masika. Sakafu ya banda iwe juu zaidi ya usawa wa nje.
Paa linaweza kuezekwa kwa mabaki ya vipande vya bati , madebe na kama
ikishindikana tumia nyasi zinazofaa kwa ajili ya kuezeka nyumba katika
eneo hilo.
NAFASI YA KUFANYA KAZI:
Banda la kuku lisiwe na nguzo au mbao nyingi sana
ndani kiasi cha kumfanya mhudumiaji wa kuku ashindwe kufanya kazi zake.
Hali hiyo itamfanya apoteze muda mwingi katika kuzizunguka nguzo hizo,
hasa wakati wa kuokota mayai au kufanya usafi.
VIFAA:
Unapotaka kujenga banda la kuku kwanza kabisa tayarisha vifaa vinavyotakiwa. Vitu kama miti au nyasi, nyavu au fito, misumari au kamba ni muhimu kuviandaa mapema.
Pili ni lazima uwe na plani/ramani kamili ya banda
hilo. Kwa wastani kila kuku anahitaji nafasi ya Meta za eneo la 0.11
hadi 0.22 (futi 1 hadi 2 za eneo.) kutegemeana na umri wa kuku.
UJENZI RAHISI:
Kuku wafugwao hatimaye ni lazima wafidie gharama za
Ujenzi wa mabanda na chakula. Gharama zikiwa kubwa sana huenda ukaifanya
shughuli ya ufugaji isiwe na faida hata kidogo hali hiyo itamfanya
mfugaji aone ufugaji hauna maana yoyote kwake. Lakini ukijenga banda
lako kwa kutumia vifaa vinavyopatikana kwa urahisi utaongeza faida zaidi
kwakuwa umepunguza gharama za uendeshaji wa mradi.
VIPIMO:
Banda la
kuku linatakiwa liwe na Meta 15 hadi meta 22 za eneo yaani Meta 3 hadi
4.5 za upana kwa meta 5 za urefu. Banda hili linaweza kutunza kuku 100
wakubwa kwa wakati mmoja.
HITIMISHO;
· Ujenzi wa mabanda unasisitizwa katika kuboresha ufugaji wa kuku wa asili ili;
· Kuongeza
uzalishaji na kupunguza vifo vya vifaranga kwa majanga mbalimbali kama
vicheche ,mwewe, mapaka, mbwa na wizi wa kuku wanaozurura holela.
· Vile
vile inatarajiwa kwamba kuku wanaozuiliwa kwenye banda na kuwekewa
chakula mchanganyiko wataongeza uzalishaji kwa kiasi kikubwa.
UTAGAJI NA UATAMIAJI WA MAYAI:
a. Kuku
huanza kutaga wakiwa na umri wa majuma 22-32 baada ya kuzaliwa
kutegemeana na ukoo ,afya na lishe.Kwa kawaida kuku wa kienyeji /asili
watachelewa kutaga kuliko wa kisasa . Matetea hufikia kiwango cha juu
cha utagaji wakiwa na umri wa wiki 40-50 na baada ya umri huo utagaji
huanza kupungua kidogokidogo. Hali hiyo inapoanza kujitokeza wafugaji
wanashauriwa kuuza au kuchinja kuku waliofikia umri huo.
b. Kuku
wanaotaga ni lazima wapate chakula chenye madini ya chokaa ya kutosha.
Chakula hiki kinaweza kuboreshwa kwa kuongezewa maganda yaliyosagwa ya
mayai na ya konokono
c. wapatie
viota vya kutagia katika mabanda yao , kwa njia hii ni rahisi kuyapata
mayai na pia mayai yanakuwa safi. ilikuwafundisha kuku kutaga kwenye
viota unaweza kuweka mayai machache katika kiota au mawe yanayofanana
na mayai . kuku wanapoaanza kuatamia hukoma kutaga , kutokana na kuokota
mara kadhaa kwa siku unaweza kuepuka kuku kutaka kuatamia .unashauriwa
kutenga mara moja matetea wanaoanza kuatamia
kwa kuwaweka katika kibanda kidogo kilichotulia akae pekee yake sehemu isiyo na kiota kwa siku chache.
d. joto la kadri kwa kuku wanaotaga ni kati ya 18ºC -29ºC.
Mauzo ya mayai:
1. Hakikisha unafanya utafiti kabla ya kuanza kufuga.
2. Uza mayai kwa kuzingatia viwango kama vile rangi, ukubwa na maumbile yake.
3. uza
mayai safi kwa kuhakikisha unapanga mayai safi kwenye trei na yale
ambayo ni machafu unayasafisha kwa kupanguza na pamba au kitambaa
kilicholowekwa maji yasiyo na sabuni( kitambaa kisiwe kimetota maji).
Mayai haya yasafishwe kabla ya kuuzwa.
4. Punguza
uvunjaji na uchafuzi wa mayai. Hii inawezekana tu pale
utakapohakikisha unatengeneza viota vya kutagia na kuyaokota mara kwa
mara. Inapendekezwa uokote mayai mara tatu kwa siku. Asubuhi wakati
kulisha mchana na jioni. Kuvunjika kwa mayai huongeza hasara kwa mradi
na kuchafua matrei ya kutunzia .
Kuatamia.
Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa ilhali bata hutotoa baada ya siku 28.
Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga:
Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya;
1) Umri
wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe
yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo
hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga
yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5).
2) Ili
kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa)
yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku
wanaohusika.
3) Ganda
la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa kwani likiwa na nyufa
yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa
au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo
husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa.
4) Hifadhi
mayai ya kuangua kwenye makasha makavu ndani ya shimo lililopo ardhini
katika sehemu yenye ubaridi kuliko sehemu zote ndani ya chumba.
5) Kabla
mayai hayajaatamiwa chunguza mayai ambayo yana mbegu na yale yasiyo na
mbegu . Mayai ya kuku aliyepandwa na jogoo yanakuwa na mtandao wa
mishipa ya damu mapema sana ambayo inaweza kuonekana kwa kutumia mwanga
mkali wa kurunzi.
6) Kabla
mayai hayajaatamiwa chunguza mayai ambayo yana mbegu na yale yasiyo na
mbegu . Mayai ya kuku aliyepandwa na jogoo yanakuwa na mtandao wa
mishipa ya damu mapema sana ambayo inaweza kuonekana kwa kutumia mwanga
mkali wa kurunzi.
7) Baada
ya mayai kuatamiwa kwa siku saba hadi kumi yanaweza kuchunguzwa mayai
yasiyorutubushwa na yenye viini vilivyokufa yanaweza kutambuliwa katika
siku saba baada ya kuanza kuanguliwa
8) Wakati
wa kupima kwa kutumia mwanga wa kurunzi mayai yaliyorutubishwa yanakuwa
na mishipa ya damu inayoonekana, na doa jeusi ambalo ndicho kiini cha
uhai.
9) Iwapo kiini cha uhai kimekufa, kinaoonekana kama kitu cha mviringo mfano wa pete kuzunguka kiini hai.
10) Mayai
ambayo hayajarutubishwa yanakuwa na nafasi kubwa ya hewa na kiini cha
uhai kinaoonekana kama kitu cheusi ndani ya ndani ya yai.
Mayai
ambayo hayajarutubishwa na yale yenye viini vilivyorutubishwa inabidi
yatengwe na kuondolewa ili yasije yakaozea ndani ya kiota, yakapasuka na
kuharibu mayai mazuri ambayo yapo katika kuatamiwa.
1) Kuku anayeatamia atengwe katika kundi ili asisumbuliwe na kuku wengine ,
2) Mtengee kuku kiota ambacho kinampa nafasi ya kupata maji safi na chakula kwa karibu.
3) Kiota au kikapu ni lazima kiwe kikubwa kiasi cha kumpa kuku nafasi ya kuatamia mayai yote.
4) Weka matandazo makavu ambayo ni mapya yaliyonyunyizwa majvu kidogokuzuia visumbufu.
5) Iwapo
vifaranga wanaototolewa ni wachache njia nzuri ya kuatamia mayai ni
kumtumia kuku kuliko mashine ya kutotolesha vifaranga kwasababu kuku ana
uwezo mkubwa wa kutotoa vvifaranga kwa asilimia 80- 100 ukilinganisha
na mashine ambayo hutotoa mayai kwa asilimia 60-80 tu.
Vifaranga vikishatotolewa
vinaweza kulelewa kwa kumtumia mama ikiwa ni wachache. Lakini vifaranga
wanaweza kulelewa kwa kutumia kifaa maalum ya kulelea vifaranga...............................................................................................................................
