Zifahamu Sababu kuu ,Kwanini vifaranga hufa?



  • KWANZA tambua vifaranga hupendelea kukaa juu, hivyo unatakiwa ujenge banda la ghorofa moja.
  • PILI tambuwa vifaranga havipendi giza wakati wa mchana, hivyo unatakiwa unapojenga ghorofa yao hakikisha ubavu mmoja una wavu unaopitisha mwanga wa jua. 
  • TATU tambuwa vifaranga havitakiwi kuishi pasipo ya mama yao, hivyo hakikisha unapowatenga vifaranga usiwaache pasipo ya mama(hata kama vipo ishirini waweke na mama mmoja tu).
  • NNE tambuwa vifaranga havitakiwi kupewa maji mengi, hivyo unatakiwa kuwapatia maji machache kwenye vyombo vidogo ambavyo havitaweza kumzamisha.
  • TANO tambua banda la vifaranga linatakiwa maranda ili kuongeza joto.
  • SITA tambuwa vifaranga vinatakiwa vifungiwe ndani kwa miezi miwili pekee.
  • SABA vifaranga havitakiwi kushikwa shikwa na mikono yako kila siku.
  • NANE vifaranga vinatakiwa kulishwa starter (nafaka nyembamba) na maziwa kwa kiasi.
  • TISA banda la vifaranga hutakiwi kulisafisha kila siku, hakikisha unasafisha mara tatu tu kwa wiki.

................
*UJUMBE usikate tamaa katika ufugaji mana hakunaga mwanzo mrahisi, changamoto ni mapito tu, jiamini mana hata wewe unaweza.* 
......................................................................................................................................


Previous Post Next Post